KWA MAELEZO ZAIDI

TANGAZA HAPA NA PATA HABARI ZA MICHEZO, KITAIFA NA KIMATAIFA HAPA VIJANA KWANZA BLOG. WASILIANA NASI: PHONE: +255 764 251 064

KWA MAELEZO ZAIDI

TANGAZA HAPA NA PATA HABARI ZA MICHEZO, KITAIFA NA KIMATAIFA HAPA VIJANA KWANZA BLOG. WASILIANA NASI: PHONE: +255 764 251 064

KWA MAELEZO ZAIDI

TANGAZA HAPA NA PATA HABARI ZA MICHEZO, KITAIFA NA KIMATAIFA HAPA VIJANA KWANZA BLOG. WASILIANA NASI: PHONE: +255 764 251 064

KWA MAELEZO ZAIDI

TANGAZA HAPA NA PATA HABARI ZA MICHEZO, KITAIFA NA KIMATAIFA HAPA VIJANA KWANZA BLOG. WASILIANA NASI: PHONE: +255 764 251 064

KWA MAELEZO ZAIDI

TANGAZA HAPA NA PATA HABARI ZA MICHEZO, KITAIFA NA KIMATAIFA HAPA VIJANA KWANZA BLOG. WASILIANA NASI: PHONE: +255 764 251 064

Tuesday, July 31, 2012

ORODHA YA WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA MAFUNZO YA UALIMU NGAZI YA STASHAHADA MWAKA WA MASOMO 2012/2013

 WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI
ORODHA YA WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA MAFUNZO YA UALIMU NGAZI YA STASHAHADA  MWAKA WA MASOMO 
2012/2013


MAELEKEZO MUHIMU
Waombaji waliochaguliwa kujiunga na mafunzo ya ualimu ngazi ya Stashahada katika mwaka wa masomo 2012/13 wanatakiwa kuripoti katika vyuo walivyopangiwa tarehe 12/08/2012. 

Kwa wale watakaochelewa kupata barua za maelekezo (Joining instruction) kutoka vyuoni wanatakiwa waripoti vyuoni katika tarehe iliyopangwa bila kukosa.
Wanafunzi wanatakiwa kufika vyuoni wakiwa na mahitaji yafuatayo:
1.Vyeti halisi vya Baraza la Mitihani la Tanzania Kidato cha NNE na SITA kulingana na kozi husika.


2. Ada kwa mwaka ni shilingi 200,000/=.  (Muhula wa kwanza shilingi  100,000/=  na muhula wa pili shilingi 100,000/=).


3.Sare ya Chuo kulingana na maelekezo ya chuo husika na


4. Fedha  kwa matumizi binafsi.


Aidha, kila Mkuu wa Chuo anatakiwa kuhakikisha wanafunzi wanaosajiliwa chuoni ni wale waliopo kwenye orodha hii tu na  SI vinginevyo.



Wednesday, July 25, 2012

WAZIRI WA UCHUKUZI DR. HARRISON MWAKYEMBE AZINDUA HUDUMA MPYA ZA SHIRIKA LA NDEGE LA QATAR KUTOKA KIA.

Picha ya pamoja mara baada ya Shirika la ndege la serikali ya Qatar (Qatar airways) leo kuzindua  huduma ya safari zake za anga kutoka Kilimanjaro kuelekea sehemu mbalimbali za dunia kila siku na kufanya huduma za safari za anga kufikia zaidi miji 118.
Mgeni rasmi katika uzinduzi huo,waziri wa mawasiliano na uchukuzi Dr. Harrison Mwakyembe akimkabidhi Mkurugenzi mtendaji wa masoko wa shirika hilo Bw. Marwan Koleilat  kwa niaba ya shirika hilo la ndege la Qatar zawadi ya picha yenye kivuli cha Mlima Kilimanjaro .
Mkurugenzi mtendaji wa masoko wa shirika la Qatar Bw. Marwan Koleilat  kwa niaba ya shirika hilo akimpa Mgeni rasmi katika uzinduzi huo,waziri wa mawasiliano na uchukuzi Dr. Harrison zawadi  ya yenye nembo ya ndege ya shirika hilo la Qatar.
Mgeni rasmi katika uzinduzi huo,waziri wa mawasiliano na uchukuzi Dr. Harrison akizungumza mbele ya wageni waalikwa wakiwemo na wahariri wa habari kutoka vyombo mbalimbali (hawapo pichani),mapema leo kwenye uwanja wa ndege wa Kimataifa KIA.
Mkurugenzi mtendaji wa masoko wa shirika la Qatar Bw. Marwan Koleilat  kwa niaba ya shirika hilo akizungumza mbele ya wageni waalikwa wakiwemo na wahariri wa habari kutoka vyombo mbalimbali (hawapo pichani),mapema leo kwenye uwanja wa ndege wa Kimataifa KIA.
Kutoka kulia ni Mkurugenzi mtendaji wa masoko wa shirika la Qatar Bw. Marwan Koleilat,Waziri wa Uchukuzi Dr.Harrison Mwakyembe,Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya KADCO, Balozi Hassan Omar Gumbo Kibelloh pamoja na Waziri wa Maliasili na Utalii Balozi Khamis Kagasheki wakijadiliana jambo.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya KADCO, Balozi Hassan Omar Gumbo Kibelloh lakizungumza machache na pia kumkaribisha mgeni rasmi na wageni waalikwa mbalimbali waliofika kwenye hafla hiyo mapema leo iliofanyika kwenye uwanja wa KIA.
 Wakuu wa uzinduzi wakipga makofi kwa pamoja mara baada ya uzinduzi huo.
Mgeni rasmi katika uzinduzi huo,waziri wa mawasiliano na uchukuzi Dr. Harrison akipiga makofi wakati kikundi cha ngoma za asili kikitumbuiza,shoto kwake ni Mkurugenzi mtendaji wa masoko wa shirika la Qatar Bw. Marwan Koleilat 
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya KADCO, Balozi Hassan Omar Gumbo Kibelloh akimkaribisha Mkurugenzi mtendaji wa masoko wa shirika la Qatar Bw. Marwan Koleilat mara baada ya kuwasili na ndege ya shirika hilo aina ya Ndege namba QR546,shoto kwake ni  Waziri wa Maliasili na Utalii Balozi Khamis Kagasheki.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya KADCO, Balozi Hassan Omar Gumbo Kibelloh akimpokea Mgeni rasmi,Waziri wa Uchukuzi Dr Harrison Mwakyembe mara baada ya kuwasili KIA tayari kwa uzinduzi 
Mgeni rasmi,Waziri wa Uchukuzi Dr Harrison Mwakyembe akishuka kwenye ndege ya Qatar kwenye Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) akiwa ameambatana na Mkewe pamoja na  Waziri wa Maliasili na Utalii Balozi Khamis Kagasheki.
 Ndege ya Qatar ikiwasili kabla ya kuzinduliwa rasmi KIA.
 Ikifanyiwa shower kwa mbwembwe zote.
 Wageni waalikwa mbali mbali wakisubiri kushuhudia uzinduzi huo.
Pichani kulia ni Mkuu wa wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro Mhe.Novatus Makunga akizungumza jambo  na Mhariri Mkuu wa gazeti la Tanzania Daima,Bw.Absalom Kibanda.
Baadhi ya Wanahabari Waandamizi wakiwa kwenye uzinduzi huo mapema leo kwenye uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA).
 
 

NIGERIA U20 YAWASILI KUIKABILI NGORONGORO HEROES.


 
Kikosi cha timu ya Taifa ya Vijana U20 ya Nigeria (Flying Eagles).
Timu ya Taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 20 ya Nigeria (Flying Eagles) inatarajia kuwasili nchini leo (Julai 25 mwaka huu) saa 10 jioni kwa ndege ya RwandAir ikiwa na msafara wa watu 30 wakiwemo wachezaji 18.
Flying Eagles itapambana na Ngorongoro Heroes katika mechi ya kwanza ya raundi ya pili itakayofanyika Jumapili (Julai 29 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 10 kamili jioni.
Mechi hiyo ya kuwania tiketi ya kucheza fainali za 18 za Afrika kwa vijana wenye umri chini ya miaka 20 zitakazochezwa mwakani nchini Algeria itachezeshwa na waamuzi kutoka Kenya wakati Kamishna ni Charles Masembe kutoka Uganda.
Flying Eagles inayofundishwa na kocha John Obuh, jana (Julai 24 mwaka huu) ilicheza mechi ya kirafiki na Rwanda (Young Amavubi) kwenye Uwanja wa Amahoro jijini Kigali. Nigeria ililala bao 1-0.
Msafara wa timu hiyo unaongozwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Ufundi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Nigeria (NFF), Chris Green. Baadhi ya wachezaji walioko katika kikosi cha Flying Eagles ni Chidi Osuchukwu, Alhaji Gero, Shehu Abdullahi, Aminu Umar, Aliyu Mohamed, Uche Agbo, Jonah Usman, Harrison Egbune, Hassan Abubakar na Yahya Adamu.
Viingilio katika mechi hiyo vitakuwa sh. 3,000 kwa viti vya rangi ya chungwa, bluu na kijani wakati VIP B na C itakuwa sh. 5,000. Kiingilio kwa VIP A itakuwa sh. 10,000.
NUSU FAINALI KOMBE LA KAGAME
Nusu fainali zote mbili za kuwania Klabu bingwa Afrika Mashariki na Kati (Kombe la Kagame) mwaka 2012 zinachezwa kesho Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kwa viingilio vya sh. 5,000, sh. 7,000, sh. 15,000 na sh. 20,000.
Azam na AS Vita ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) zitacheza nusu fainali ya kwanza kuanzia saa 8 kamili mchana, na kufuatiwa na nusu fainali ya pili kati ya Yanga na APR ya Rwanda itakayoanza saa 10 kamili jioni.

 Habari toka

SAJUKI APATA GONJWA BAYA LAMSHAMBULIA UTI WA MGONGO

 
Sadick Juma Kilowoko ‘Sajuki’.
 
Sadick Juma Kilowoko ‘Sajuki’ akiwa na mkewe Wastara.
PAMOJA na kwamba afya ya staa wa filamu Bongo, Sadick Juma Kilowoko ‘Sajuki’ inaendelea vizuri, imegundulika kuwa ana ugonjwa mwingine tofauti na ule uliompeleka India kufanyiwa upasuaji,
Hivi karibuni, Sajuki alirejea kutoka nchini India alipokwenda kwa ajili ya matibabu ambapo alionekana kuwa na mabadiliko makubwa kiafya jambo lililowapa matumaini mashabiki wake.

HABARI MEZANI
Akizungumza na waandishi wetu, juzi, Jumapili nyumbani kwake, Tabata jijini Dar es Salaam, mke wa Sajuki, Wastara Juma alisema mumewe amegundulika kuwa na tatizo lingine walipokuwa nchini India kwa matibabu.
Alisema, hawakutaka kuweka hali hiyo mapema kwa Watanzania kwa kuhofia kusababisha simanzi, lakini sasa wanalazimika kufanya hivyo ili kuwafanya wajue kinachoendelea kwa staa wao.
“Kwa kweli mume wangu bado anaumwa na amegundulika kuwa na tatizo lingine ila tunamshukuru Mungu anaendelea vizuri,” alisema Wastara kwa huzuni nyingi.

NI UGONJWA GANI?
Kwa mujibu wa Wastara, walipokuwa India (katika Hospitali ya Apollo), Sajuki alifanyiwa vipimo mbalimbali ili kubaini matatizo yanayomsumbua ambapo aligundulika kuwa na tatizo kwenye uti wa mgongo na ngozi ya mwili mzima.
“Ana tatizo kwenye mfupa wa uti wa mgongo, lakini pia anasumbuliwa na tatizo jingine kwenye ngozi. Baada ya madaktari kugundua magonjwa hayo walimuanzishia dawa ya kutibu mgongo na mazoezi kwa ajili ya kumuweka sawa.
“Hizo dawa alianza kuzitumia tulipokuja huku, ambapo pia anaendelea na mazoezi. Tatizo lingine ni hilo la ngozi, ambalo pia anaendelea kutumia dawa,” alisema.

KWA NINI MGONGO?
Akifafanua kuhusu ugonjwa unaoshambulia sehemu ya mfupa wa uti wa mgongo, Wastara alisema madaktari walisema, tatizo hilo linasababishwa na kukaa kwa muda mrefu.
“Jambo hilo tulikubaliana nalo, kwa sababu ni kweli Sajuki huwa anakaa muda mrefu kwenye kompyuta kwa ajili ya kazi zake, lakini pia huwa anaendesha gari kwa muda mrefu. Tunaamini ndiyo chanzo cha ugonjwa huo kama madaktari walivyosema,” alisema na kuongeza:
“Lakini baada ya kupata dawa na ushauri  sasa anaendelea vizuri,  kwa sababu pia anafuata masharti aliyopewa vizuri. Huwa nahakikisha anapata muda mrefu wa kupumzika, hakai muda mwingi na haendeshi sana gari.
“Wamemwambia mambo mengi, hata kuinainama kila mara pia wamekataza. Kimsingi mwenzangu anahitaji uangalizi wa karibu sana. Hata hivyo anaweza kuendelea na filamu ila kwa kuzingatia na scene (onesho) yenyewe, ila kwa sasa anapumzika kwanza ili afya yake itengemae.”

KLINIKI KILA WIKI
Akiendelea kuzungumzia afya ya mumewe, Wastara alisema huwa wanalazimika kwenda Kliniki ya kila wiki katika hospitali moja jijini Dar es Salaam kwa lengo la kuangaliwa maendeleo yake.
Aidha, alisema kila wiki tatu huwa wanatuma vipimo nchini India katika Hospitali ya Apollo aliyokuwa akitibiwa kwa lengo la kuchunguza maendeleo yake.

KUHUSU UGONJWA WA NGOZI
Wastara alisema, tatizo la ngozi alilonalo mumewe bado hajaanza kutumia dozi yake kwa sababu hawajapata fedha ya kutuma India ili waweze kutumiwa dawa zenyewe.
“Tupo kwenye mchakato wa kutafuta hizo fedha, lakini hali bado ni ngumu na anatakiwa kuanza dozi mapema kama madaktari walivyoshauri,” alisema na kuongeza:
“Mwezi Desemba (mwaka huu) anatakiwa kurudi tena ili aangaliwe tena maendeleo yake kwa ujumla. Yote hiyo ni gharama kubwa sana, lakini tunaamini Mungu atatusimamia.”

GHARAMA ZAMTOA CHOZI WASTARA
Alisema kwa namna mahitaji yalivyo mengi na yanayohitaji fedha, wapo kwenye wakati mgumu kuweza kuyakabili.
“Kiukweli bado tunahitaji msaada wa Watanzania wenzetu. Tunashukuru kwa wale waliojaliwa kutusaidia awali hadi kufanikisha safari yetu ya matibabu India lakini watakaoguswa wanaweza kuendelea kutusaidia.
“Mpaka sasa Sajuki hajaanza dozi ya ugonjwa wa ngozi na zipo nyingine anazotakiwa kuzitumia, lakini hazipatikani hapa...ni mpaka India.”

VIDUME VYAMTOKEA WASTARA
 Akizungumzia suala la usumbufu wa kimapenzi, Wastara alisema ni jambo la kawaida na ni kweli kuna baadhi ya wanaume wanatumia udhaifu wa ugonjwa wa mumewe kumshawishi kimapenzi.
“Kutongozwa ni jambo la kawaida kwa mwanamke, lakini mimi kama Wastara msimamo wangu ni kumheshimu mume wangu. Siwezi kushawishika kwa namna yoyote, kwanza hata hamu yenyewe sina.
“Ninachokiangalia kwa sasa ni afya ya mume wangu. Najua nina wajibu mkubwa wa kuhakikisha namhudumia mume wangu kwa mapenzi yote. Akili yangu haipo kwenye mapenzi kabisa, hali aliyonayo mume wangu inaniumiza sana.
“Kamwe sitamsaliti Sajuki wangu. Wema wake kwangu wakati nikiwa kwenye matatizo siwezi kuulipia kwa kumdhalilisha kwa kutoka na mwanaume mwingine eti kwa sababu anaumwa. Anayewaza kufanya hivyo, akajaribu kwingine, siyo kwangu.”

KALAMU YA MHARIRI
Kwa matatizo aliyonayo Sajuki ni wazi yeye na familia yake bado wanahitaji msaada wa hali na mali ili kuweza kukidhi mahitaji ya matibabu yanayomkabili kwa sasa.
Kama Mtanzania mwenzake, guswa na moyo wa utoaji na Mungu wa Mbinguni atakuongezea katika mifuko yako.
Ikiwa umeguswa, tafadhali tuma mchango wako kwenye akaunti namba 050000003047 yenye jina la Wastara Juma Issa iliyopo katika Benki ya Biashara ya Akiba (ACB) au tumia Tigopesa kwenda namba 0713 666113 yenye jina Wastara Juma.

Saturday, July 7, 2012

WEMA SEPETU, JACQUELINE WOLPER HAKUNA MBABE

 Wema akijifua.

 Wolper.
Wasanii mahiri wa Filamu, Wema Sepetu na Jacqueline Wolper wakijifua kabla ya mpambano wao leo.
 Mwamuzi akiamua mpambano uanze.

 Wolper na Wema wakionyeshana ubabe.

Wema akipata mawaidha kutoka kwa mwalimu wake Rashid Matumla.
Waigizaji mahiri wa filamu nchini, Wema Sepetu na Jacqueline Wolper wametoka suruhu katika mpambano wao wa raundi 2 uliofanyika katika Uwanja wa Taifa jijini Dar e Salaam kwenye Tamasha la Usiku wa Matumaini.

http://irenemwamfupejamii.blogspot.com/

SIMBA WAIKANDAMIZA YANGA KWA PENALTI 3-2


 Simba wakiingia uwanjani kupasha misuli.

 
 Yanga wakijichua kwa ajili ya mtanange na watani wao wa jadi Simba.
Mechi ya watani wa jadi
 Wachezaji wa Yanga na Simba (Wabunge) wakiimba wimbo wa Taifa kabla ya mechi kuanza.
Zitto Kabwe akitoa pasi.

BONGO MOVIE WAICHACHAFYA BONGO FLEVA 1 - 0

 Benny Kinyaiya na JB wakishangilia.


Wachezaji wa Bongo Movie na mashabiki wake wakishangilia bao lao lililofungwa na Kiduko.

TANZANIA NA MSIMAMO WAKE JUU YA NDOA ZA JINSI MOJA



Tanzania stands firm on aid-gay rights spat with UK
By Fumbuka Ng'wanakilala | Reuters – Fri, Nov 4, 2011

DAR ES SALAAM (Reuters) - Tanzania has become the latest African government to say it will not legalise homosexuality even if that means it loses substantial financial aid from Britain.
Government officials reacted strongly to Prime Minister David Cameron's threat to cut aid to countries that deny gay rights.

"Tanzania will never accept Cameron's proposal because we have our own moral values. Homosexuality is not part of our culture and we will never legalise it," foreign affairs minister Bernard Membe was quoted as saying by Tanzania's Guardian newspaper.

"We are not ready to allow any rich nation to give us aid based on unacceptable conditions simply because we are poor. If we are denied aid by one country, it will not affect the economic status of this nation and we can do without UK aid."

Tanzania, a former British colony and one of Africa's biggest per capita aid recipients, received $453 million (282 million pounds) of aid for its 2011/12 budget, with Britain the largest provider of general budget support.


Ghana's President John Atta Mills said Wednesday his government would never legalise homosexuality. Uganda has also reacted strongly to Cameron's comments.

The Department for International Development (DFID) gave Tanzania 144 million pounds in aid in 2009/10 and has pledged to spend an average of 161 million pounds per year in Tanzania until 2015.

Homosexuality is a serious criminal offence in Tanzania, punishable by imprisonment, but no one has been prosecuted.

"We cannot be directed by the United Kingdom to do things that are against our set laws, culture and regulations," Membe was quoted as saying.

Zanzibar President Ali Mohamed Shein also rejected the British demands for gay rights to be respected in Tanzania.

"We have strong Islamic and Zanzibari culture that abhors gay and lesbian activities, and to anyone who tells us that development support is linked to accepting this we are saying no," Shein told journalists Thursday.
Zanzibar, Tanzania's semi-autonomous archipelago, enacted a law in 2004 banning homosexual relations. Male offenders face more jail time, up to 25 years, than convicted women.

Homosexuality is illegal in 37 African countries, and rights groups say gays are often the targets of violent hate campaigns.

Friday, July 6, 2012

SASA UNAWEZA KUTOA MAONI YAKO KUHUSU KATIBA KUPITIA UKURASA WA FACEBOOK WA TUME.

 
Sasa tunaweza kuwasilisha maoni kuhusu Katiba Mpya, kupitia Facebook (bofya hapa), kwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba kwa akaunti ya iliyoanzishwa kwa jina  Tume ya Mabadiliko ya Katiba Tanzania https://www.facebook.com/pages/Tume-ya-Mabadiliko-ya-Katiba-Tanzania/323414977745643